NGUVU YA HABARI

Monday, June 18, 2012

Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima: LEO NI SIKU YA MTOTO WA AFRIKA NI KWELI WATOTO WANAPEWA HAKI ZAO ?

Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima: LEO NI SIKU YA MTOTO WA AFRIKA NI KWELI WATOTO WANAPEWA HAKI ZAO ?

maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika jijini Mwanza leo ~ MTAA KWA MTAA

         TAARIFA YA MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA
      YALIYOFANYIKA KIMKOA KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA,
                HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA 16/6/2011
 1.0   Utangulizi
     Siku ya siku ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa tarehe 16, Juni ya kila mwaka.
     Siku hii inaadhimishwa kwa Azimio la nchi 51 wanachama wa uliokuwa Umoja wa
     Nchi huru za Afrika (OAU) kwa ajili ya kukumbuka mauaji ya kinyama
     waliofanyiwa watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini mnamo
     mwaka 1976. Hapa nchini kuna utaratibu wa kuazimisha Kitaifa kila baada ya
     miaka mitano, mwaka huu maadhimisho yamefanyika Kimkoa. Kwa Mkoa wa Dar
     es Salaam maadhimisho haya yalifanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,
     Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Hii ni kutokana na utaratibu tuliojiwekea wa
     kuadhimisha kwa kila mwaka kwa awamu katika Halmashauri za Manispaa za
     Mkoa wa Dar es salaam.
 2.0   Lengo la Maadhimisho
     Siku hii huadhimishwa kwa lengo la kukumbuka mauaji ya kinyama waliofanyiwa
     watoto nchini Afrika ya Kusini wakati wakidai haki zao za msingi, pia
     kuwakumbusha wazazi/walezi na jamii kwa ujumla juu ya haki na wajibu wa
     jamii katika kuwalea watoto. Aidha, hutoa nafasi ya kuwakumbusha watoto haki
     na wajibu wao kama watoto katika Taifa.
 3.0   Kauli mbiu
     Kauli mbiu ya mwaka huu (2011) inasema “Tuungane Pamoja Kuchukua
     Hatua za Haraka Kushughulikia Tatizo la Watoto Wanaoishi Mitaani”.
     Ikiwa na maana ya kukumbusha umuhimu wa wazazi, walezi wadau wote katika
     kushughulikia tatizo la watoto wanaoishi mitaani na kwamba watoto hawa ni
     wetu na ndio msingi mkubwa wa kuleta maendeleo ya nchi hii kwa siku za
     baadae. Hivyo basi, jamii tunao wajibu kipekee wa kumuandaa mtoto wa taifa
     hili ili awe raia mwema.
 4.0   Yaliyojitokeza
     • Risala ya watoto
     • Hotuba ya Mgeni rasmi
     • Vikundi vya burudani
     • Mgeni rasmi kutembelea mabanda
4.1  Risala ya watoto
     Watoto walipata nafasi ya kusoma risala mbele ya Mgeni rasmi, wazazi, walezi na
     wadau mbalimbali ambayo iliwasilishwa kwa niaba ya watoto wenzao wa Mkoa
     wa Dar es salaam. Katika risala yao watoto walimshukuru mgeni rasmi kwa
    kukubali kuungana nao katika maadhimisho hayo. Risala hiyo ilitoa ujumbe
    mbalimbali ikiwa ni pamoja na;-
           Jamii kuweka utaratibu wa kuwahudumia watoto wote bila kubagua
        •
           Serikali iangalie namna ya kuondoa umaskini wa kipato katika ngazi ya
        •
           familia
           Baadhi ya watu katika jamii waache tamaa ya kuchukua mali na kuwaacha
        •
           watoto wakihangaika mitaani pindi wazazi wao wanapofariki dunia.
    Pia, risala ilibainisha vyanzo vya watoto kwenda kuishi mitaani kama vile,
    kutopata upendo kutoka kwa wazazi na walezi, matatizo mimba za utotoni, utoro
    shuleni na tamaa. Hivyo jamii na watoto wanapaswa wafahamu haki na wajibu
    wao.
4.2 Hotuba ya Mgeni rasmi
    Hotuba ya Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Said Meck
    Sadick katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ilisomwa na Ndugu E.
    Ntandu Katibu Tawala Msaidizi Idara ya Mipango na Uratibu aliyemwakilisha
    Kaimu Mkuu wa Mkoa katika maadhimisho hayo. Katika hotuba yake Mgeni rasmi
    aliwashukuru Wataalamu wa Sekretarieti na Halmashauri za Manispaa katika
    kuandaa siku hiyo. Aidha, alitoa Shukrani za dhati kwa Shirika la AMREF, Benki
    ya CRDB, Benki ya Wananchi, Shirika lisilo la kiserikali la Dar Urban Plan na
    Wadau wengine wote kwa kutambua mchango wao katika kuadhimisha siku ya
    Mtoto wa Afrika ndani ya Mkoa wetu. Pia alisisitiza kwamba kwa mwaka ujao
    wazazi na walezi wengi wahamasishwe ili waungane pamoja na watoto wao
    katika kuadhimisha siku hiyo ili ujumbe unapotolewa uweze kuwafikia.
           Mgeni rasmi alitoa wito kwa jamii itimize wajibu wake kama kauli mbiu ya
    mwaka huu unavyotutaka na kuahidi kwamba Mkoa utaendelea kutoa fursa kwa
    watoto ili kuweza kutoa maoni yao kwa Maendeleo ya Taifa na kuwachukua
    hatua kali za kisheria wale wote wanaoendeleza ukatili dhidi ya watoto.
    Vikundi vya burudani.
4.3
    Watoto walipata nafasi ya kuonesha burudani mbalimbali kwa Mgeni rasmi na
    watu wote waliofika katika viwanja vya Mnazi Mmoja. Burudani hizo zilikuwa ni
    pamoja na Ngoma ya mganda, kwaya na maigizo zikiwa zimebeba ujumbe
    mbalimbali kama vile, ajira za watoto zikomeshwe na wazazi na walezi
    wapelekwe watoto shuleni kwani uridhi pekee wa wazazi kwa watoto ni elimu,
    jamii iwalee na kuwatunza watoto. Aidha, Serikali iendelee kutoa elimu kwa jamii
    juu ya haki na wajibu wa watoto na jamii.
4.4  Mgeni rasmi kutembelea mabanda
     Mgeni rasmi alipata nafasi ya kutembelea mabanda ambayo yalishehenezwa na
     kazi mbalimbali za watoto zikiwemo; - picha za kuchora, vifaa vya kufinyanga
     kwa udongo (kinu na kibao cha kusukumia chapati), bangili za wanawake za
     kuvaa mikononi ambazo hutengenezwa na watoto wenye ulemavu wa macho.
   5 Hitimisho
     Kila mmoja wetu awajibike kwa nafasi aliyonayo katika kuhakikisha tatizo la
     watoto wanaoishi mitaani linatoweka na hatimaye kuwa na Taifa endelevu lenye
     kutekeleza na kusimamia misingi ya haki na wajibu kwa watoto.

chadema cha alika wagombe wa uchaguzi 2015

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
Katika jitihada za kujiandaa na uchaguzi mkuu wa 2015 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewataka wanachama wake wenye nia ya kugombea ubunge na udiwani kuwasilisha barua za maombi, picha, vyeti,  wasifu na jimbo wanalotaka kugombea kwenye Ofisi ya Katibu Mkuu, tayari kwa maandalizi.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema jana na kuwaagiza wanafunzi ambao ni wanachama wa Chadema wanaohitimu mwaka huu katika vyuo vikuu vya Mkoa wa Dodoma kufanya hivyo mara moja.

Akihutubia katika mahafali ya kuwaaga wanachama hao wanaosoma vyuo vikuu vya Dodoma, St. John’s na Chuo cha Biashara (CBE), Mbowe, alisema kila anayetaka kugombea awasilishe maombi na kwamba mwaka 2015 wagombea watakuwa wengi kwa kila jimbo ili kuleta ushindani.

Alisema  taarifa za wagombea hao zitafanywa kuwa siri na watakaojitokeza kugombea 2015 watapata mafunzo maalumu ya uongozi, kampeni na pia watapewa ajenda za kuzungumzia majukwaani wakati wa kampeni.

“Kama CCM ilidhani kuwa mwaka 2015 kutakuwa na jimbo au kata ambalo mgombea atapita bila mgombea, safari hii wameula wa chuya. Tumefanya operesheni Mtwara na Lindi,  tutaendelea na operesheni Dar na Pwani kisha tutaendelea Dodoma, Morogoro na Singida.

“Tunataka kujenga mtandao wa chama ngazi za chini, vijijini na mtaani kama CCM inadhani tunacheza makidamakida  watashangaa,” alisisitiza Mbowe na kuongeza kuwa lengo ni kuwatambua na kuwajenga viongozi mapema.

Katika mkutano huo, Mbowe aliwaambia wanachama wa Chadema vyuoni (Chaso) Mkoa wa Dodoma kuwa CCM inawanyanyasa wanafunzi wanaoiunga mkono Chadema na pia inanyanyasa wafanyakazi na wafanyabiashara wanaoonekana kushabikia chama hicho.

MIKAKATI YA CHADEMA

Mbowe ametangaza kuwa katika uchaguzi mkuu wa 2015 Chadema haitapokea 'maskrepa' yaliyokosa nafasi katika vyama vingine, biashara ya kupokea watu waliokosa nafasi katika vyama vingine ilikuwa 2010.

Alisema tabia ya kukimbilia meli dakika za mwisho ilikuwa zamani na kwamba uchaguzi ujao hawatakubali waliokosa fursa kwa vyama vyao kukimbilia Chadema.

Mipango yao ni  kupata wabunge na viongozi bora watakaopimwa kwa dhamira, uwezo na  uwajibikaji kwa chama.

“Wafanyakazi wanatishiwa kufukuzwa kazi na wafanyabiashara wanafilisiwa na kubambikiwa kodi kisa wameonekana kushabikia Chadema,” alisema.

Baada ya kuhutubia, wanachama wa Chadema vyuoni mkoani Dodoma wameutaka uongozi wa chuo kuondoa bango la CCM lililoko UDOM kwa maelezo kuwa ni kinyume cha Ibara ya 7 ya Sheria ya Vyuo Vikuu ya 2005.

Akisoma risala ya wanafunzi Pasquina Ferdinand mwanafunzi wa  Shahada ya Ualimu  mwaka wa pili, Chuo Kikuu cha St John’s, alisema CCM ina bango ndani ya UDOM kinyume cha sheria ya vyuo vikuu ya 2005, alionyesha kuwa ni sheria inayoihusu Chadema pekee lakini kwa CCM haina tatizo.

“Tunaomba umweleze Waziri Mkuu kama siasa haziruhusiwi vyuoni kwanini basi CCM ina bango UDOM kinyume cha sheria wapewe amri ya kuliondoa kwani UDOM siyo mali ya CCM inajengwa kwa fedha za Watanzania,” alisema.

Akijibu, Mbowe aliwataka wanafunzi wanachama wa Chadema wanaosoma UDOM kumletea taarifa za kunyanyaswa kwa itikadi yao ili azipeleke kwa Waziri Mkuu na awe na ushahidi wa kutosha ili amuulize swali bungeni.

Wakati huo huo, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Tundu Lissu, ametangaza kuwa watatumia nguvu ya umma kupinga kufukuzwa wanafunzi vyuo vikuu.

“Sisi wazazi tunawajibika kuhakikisha kuwa watoto wetu wanasoma kwa kuizuia serikali isiwanyanyase kwa kuwafukuza wakidai haki yao, hili litafanywa kwa njia ya nguvu ya umma ... tukiona wanafunzi wamefukuzwa UDOM umma uingie mitaani kuandamana kama ni Dar es Salaam watu waingie mitaani tuhakikishe kuwa hapatoshi,” alisema Lissu.


CHANZO: NIPASHE

na Henry Kapinga blog

Friday, June 15, 2012

Hapa nipo na rafiki yangu, Dick Masanja eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

katiba





Watanzania washauriwa kutumia fursa waliyonayo sasa ya kuchangia maoni ya katiba mpya ya Jamhuri ya Tanzania ambayo hawajawahi kupata tangu miaka hamsini ya uhuru wa Tanzania, kwa sasa serikali imeamua kusikia na kujibu kilio cha Watanzania kutaka kuunda katiba mpya inayoshirikisha mawazo ya wananchi badala ya kutumia katiba ambayo iliundwa na wananchi wachache.
Ushauri huo umetolewa na Meneja wa Mlimani Media, Bi. Edda Sanga wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hizi