NGUVU YA HABARI

Monday, March 24, 2014

AZAM FC, YOUNG AFRICANS, MBEYA CITY UBINGWA BADO KITENDAWILI: MASHABIKI

Na Samwel Mbugi, Mbeya.
Wadau na wapenzi wa soka jijini Mbeya wametoa maoni yao kuhusiana na msimu huu wa mashindano ya ligi kuu Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 wakilinganisha na mashindano ya msimu wa mwaka jana 2012/2013.

Wakizungumza na mtandao huu kwa nyakati tofauti walisema kuwa msimu huu ni mgumu sana ikilinganishwa na miaka mingi iliyopita timu zilizo kuwa zinaonyesha upinzani mkubwa dhidi ya Young Africans Sports Club (Yanga) na Simba Sports Club zilikuwa chache lakini msimu huu unaonesha kila timu imejipanga kuleta ushindani mkali bila kuogopa vilabu vikongwe.

Pia walisema kuwa mwaka huu haitabiriki haraka timu itakayochukua ubingwa kwani kila timu inaonekana kujianda vyema kitu ambacho kimeleta changamoto kwa timu kubwa zilizozoea kuchukua ubingwa wa mashindano ya ligi kuu Tanzania Bara.
Mpaka sasa Timu za Azam FC, Young Africans Sports Club na Mbeya City zina nafasi kila moja ya kutwaa ubingwa mwaka huu.

Bingwa mtetesi Young Africans Sports Club yupo nyuma kwa pointi 4 dhidi ya makamu bingwa Azam FC mwenye pointi 47 na akiwa na mechi moja mkononi, huku Mbeya City akiwa na Pointi 42.
Kikosi cha  wachezaji wa Jangwani Young African Sports Club wakiwa katika picha ya pamoja. Timu ya Yanga ili kutetea ubingwa inatakiwa kushinda mechi zilizobaki huku ikiombea tinu ya Azam ikifungwa ama kutoa suluhu mechi zilizobaki. (Picha Kwa msaada wa tovuti ya Young Africans Sports Club)
Wachezaji wa Young Africans Sports Club wakicheza kiduku bada ya kufunga goli la Kuongoza dhidi ya Azam FC (Picha Kwa Msaada wa Full Shangwe)
Wachezaji wa Azam FC wakishangilia goli baada ya kurudisha goli dhidi ya Yanga mechi ambayo iliisha kwa timu hizo kufungana 1:1.(Picha Kwa Msaada wa Full Shangwe)
Sambamba na hayo wengi wao walitoa ponge kwa timu ya Mbeya City kwa kuonyesha upinzani mkubwa licha ya kuwa ni mara ya kwanza kucheza mashindano hayo ya ligi kuu Tanzania Bara.

Wamezitaka timu za ligi daraja la kwanza kuiga mfano kwa timu ya Mbeya city.
Wachezaji wa Mbeya City pamoja na mashabiki wao wakishangilia ushindi wa 2:0 dhidi ya Ruvu Stars. (Picha Kwa Msaada wa Full Shangwe)

Katiba mpya itapatikana kweli Tanganyika


Sunday, March 16, 2014

ASIYEKUBALI KUSHINDA SI MSHINDANI KALENGA, IRINGA

Akina mama mkoani Iringa katika Jimbo la Kalenga wakishangilia baada ya Godfrey Mgimwa kuibuka mshindi wa ubunge jimboni hapo
Uchaguzi wa jimbo la kalenga uwe fundisho kwa chaguzi zijazo kwa vyama vya siasa na vyombo vya dola vinavyohusika kulianda Amani na usalama wa nchi pamoja na raia wake.


Godfrey Mgimwa akinyanyuliwa na mmoja wa viongozi wa CCM mkoani Iringa katika Jimbo la Kalenga baada ya kuibuka mshindi katika uchaguzi ulifanyika Machi 16 mwaka huu akirithi kiti cha ubunge kilichoaachwa wazi na baba yake baada ya kufariki dunia.

Licha ya uchaguzi wa jimbo la Kalenga kumalizika na Godfrey Mgimwa (CCM) kuibuka kidedea bado umeacha kovu lisilotibika haraka miongoni mwa walioumizwa kipindi cha kampeni za uchaguzi huo.
Katika kampeni hizo CHADEMA na CCM vilikuwa vikituhumiana kwa kuwatumia vijana katika matukio ya kiuhalifu kama vile kuwakamata viongozi wa vyama hivyo na kuwapiga na hata kuwateka viongozi hao.
CCM waliwatuhumu wafuasi wa CHADEMA kupiga na kumuumiza kiongozi wa CCM na dereva wa Naibu Waziri wa Uchumi Mwigulu Nchemba wakati CHADEMA wakiwatuhumu wafuasi wa CCM kwa kumpiga mchungaji wa kanisa la Orthodox, na kumpiga mbunge wa viti maalum wa CHADEMA Rose kwa madai alikuwa anatoa rushwa kwa wapiga kura.

Kasoro zote zilizojitokeza kipindi cha kampeni hadi uchaguzi serikali na vyama vya siasa havina budi kutafuta suluhu ya kutatua kasoro hizo ikiwemo kuwafundisha vijana wao namna ya kufanya kampeni za Amani kwa kutoa sera za kuwashawishi wananchi wamkubali mgombea badala ya kushindana kwa virungu na mapanga.
Matukio haya yote kama yatafumbiwa macho hakika yataliingiza  taifa katika machafuko ya kisiasa yasiyo na tija yoyote kwa taifa hili.
Kukomaa kwa Demokrasia si kushindana kwa kupigana bali ni kushindana kwa sera na pindi mtu anaposhindwa katika uchaguzi baada ya wananchi kuamua kumpa kura mtu mwingine, aliyeshindwa basi anakubaliana na matokeo na kumpongeza aliyepita.
Sasa baada ya wanakalenga kumchugua Godfrey Mgimwa kuwa mbunge wao, mbunge huyo hana budi kuondoa tofauti zao zote na wanachama wa vyama vya upinzania na kuwatumikia wananchi wake kwa kuhakikisha ahadi zilizo ahidi katika kipindi hiki kifupi cha uchaguzi anazitekeleza kwa muda mwafaka ilikujiwekea mazingira ya kukubalika na wananchi wa kalenga.
Wanakalenga hawakuhitaji na wala hawakumchagua kwa ngonjera za ahadi bali wamempa fursa hiyo ya kuwatumikia wananchi hao baada ya kumwona ametambua matatizo wanayokabiliwa nayo ambayo mbunge huyo atayatatua katika kipindi hiki kifupi cha mwaka mmoja.
Hata hivyo si dhambi kwa mbunge mteule Mgimwa akatimiza baadhi ya malengo ambayo yaliaachwa na marehemu Williamu Mgimwa badala ya kuongeza ahadi nyingi zisizotekelezeka kwa wanakalenmga kwa lengo tu aonekana ana ahadi na malengo mazuri kwa wananchi wa Kalenga.
Aidha, katika kampeni wanafunzi ama watoto walichukuliwa kama mfano wa kuonesha namna gani serikali ya chama tawala inavyoshindwa kuwasaidia wananchi hata wanafunzi katika kuhakikisha wanapata mahitaji muhimu ya jamii.
Ni wazi sasa aliyepita atahakikisha pia wanafunzi waliooneshwa kama mfano wa wanafunzi wanaotoka katika familia masikini wanasaidie na wanapata elimu sawa na watoto wa vigogo badala ya kuwaacha watoto katika mazingira yale yale ambayo hayaoneshi utofauti wo wote wa chama hicho kugundua kuwa watoto hao wanatoka katika familia masikini.
Hata hivyo kuna haja ya kuangalia upya sheria ya vyama vya siasa ili ifanyiwe mabadiliko kutokana na sheria hiyo kutokuwa na kikomo cha idadi ya vyama vya siasa vinavyotakiwa kusajiliwa nchini.
Kutokana na sheria hiyo kukosa meno ya imesababisha utitiri wa vyama vingi vya siasa ambavyo vinaonekana kuanzishwa kwa malengo ya kupata ruzuku ambayo inaingia mifukoni mwa watu wachache.
Ruzuku zinazotolewa kwa vyama vya siasa ni fedha za wananchi ambazo zingeweza kuwasaidia wananchi katika mambo mengine ya msingi kwa jamii.

Uwingi wa vyama vingi nchini Tanzania haumanishi kukomaa kwa Demokrasia kwa kuwa nchi zilizoendelea kama marekani ina vyama viwili tu na bado ni nchi iliyokomaa kidemokrasia.
Wapiga kura katika Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa wakiwa tayari kwa kupiga kura kumchagua mgombea wapendaye baada ya kampeni za kujinadi wagombea hao kuwashawishi wananchi hao na kuamua kwa hiari yao nani wape kura zao. (Picha kwa msaada wa Michuzi blogu)

Wednesday, March 12, 2014

ELIMU YA SIASA NA URAIA KWA VIJANA YAHITAJIKA TANZANIA



Imedai kuwa wimbi la vijana kujiingiza katika siasa limezidi kuwa kubwa huku wengi wao wakiwa na elimu duni ya siasa hali inayochangia wao kutumiwa vibaya na wanasiasa.
NGUVU YA HABARI imefanya mahojiano na viongozi wa umoja wa vijana chama cha wananchi -CUF, Baraza la Vijana la CHADEMA na wachambuzi wa masuala ya siasa ili kujua ni njia gani zinaweza kutumika ili kuhakikisha vijana wanapata elimu ya siasa kuondoka na kutumika vibaya katika mambo ya siasa.
Mwekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA), John Heche amesema  CHADEMA kimekuwa kikitumia kila njia kuhakikisha vijana wapata elimu ya siasa na kuwapa fursa vijana kugombea ngazi mbalimbali za uongozi ili kueneza elimu kwa vijana wenzao.

BOFYA HAPA KUMSIKILIZA JOHN HECHE MWENYEKITI WA BAVICHA-CHADEMA………..
JOHN HECHE akiwa katika shughuli zake za kisiasa mbele ya waandishi wa habari

Naye katibu wa Umoja wa vijana  CUF, HAMIDU BOBALI amewataka wabunge wa katiba kupitisha  baraza la vijana la taifa ambalo litawaunganisha vijana kujadili mambo mbalimbali yanayowahusu ikiwemo elimu ya siasa.

Katika mahojiano  Mchambuzi wa maswala ya siasa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk. Benson Bana amesema vijana wengi wamekuwa wakitumika kisiasa visivyo kutokana na wengi wao kukosa elimu ya uraia.
BOFYA HAPA KUMSIKILIZA DK Bana……………… 
 
Naye mchambuzi wa masuala siasa Profesa Mwesigwa Baregu alipohojiwa kwa nyakati tofauti na NGUVU YA HABARI kuhusiana na uelewa wa vijana juu ya  itikadi za vyama vya siasa amesema kuna vijana wamekuwa wakijitahidi kujifunza masuala ya siasa na kufanya tafiti mbalimbali za vyama vya siasa zinazowasaidia kujua itikadi za vyama vyao na kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya kisiasa yanayoikumba jamii inayowazunguka.
Aidha Profesa Baregu amewataka baadhi ya vijana ambao wamekuwa wakitumia muda wao mwingi kushabikia vyama ama wanasiasa bila kujua itikadi za vyama  kuachana na tabia hizo za ushabiki wa vyama vya sisiasa na badala yake wajifunze sera za vyama hivyo wanavyovipenda ili kuweza kuchambua ubora wa sera za vyama hivyo.
BOFYA HAPA KUMSIKILIZA Prof Baregu………………..
Prof. Baregu asisitiza elimu ya urai kwa vijana
Aidha profesa Baregu ameasa vyama vya siasa kutoa elimu ya siasa kwa vijana wao ili kuwawezesha  kujua imani, itikadi na sera za vyama vyao badala ya kuacha njiapanda wakielea bila kujua itikadio za vyama vyao,
Hata hivyo, vijana walipohojiwa kwa nyakati na NGUVU YA HABARI kutaka kujua nini kunawavutia kujiingiza katika masuala ya siasa kwa wingi zaidi na wana uelewa gani wa itikadi za vyama wanavyoshabikia, wamekuwa na majibu tofauti huku wengi wao wakisema ugumu wa maisha ndio unao wafanya wajiingize katika vyama vya siasa hata kama hawaelewi hatima ya maisha yao.
VIJANA WANASEMAJE............

Sunday, March 9, 2014

IMANI ZA KISHIRIKINA ZAHAMISHIA IBADA CHOONI JIJINI MBEYA, WACHUNGAJI NA WAUMINI WA PENTEKOSTE WAUNGANA NA KUWEKA KAMBI CHOONI



Waumini wa kanisa la Pentekoste Holiness Association Mission in Tanzania pamoja na wachungaji wa makanisa jirani na kijiji cha Iyunga Mapinduzi, wilaya ya Mbeya vijiji, jijini Mbeya wamefanyia ibada ibada katika eneo la choo baada ya mshirika wa kanisa hilo kuingia katika choo hicho na kukuta kimejaa nguo, madumu na chupa zenye damu pamoja na nyama zinazosadikiwa kuwa za binadamu na wanyama.
Kwa mjibu wa shuhuda watukio hilo la namna yake Eliza Subiri  amesema aliingia katika choo hicho kwa lengo la kujisaidia ndipo akaiona chupa katika shimo la choo, jambo lililomsababisha aende kwa mchungaji wa kanisa hilo na kumwambia kile achokiona.
Kama maigizo vile, baada ya mchungaji kuingia katika choo hicho akashuhudia mengi zaidi ya vile alivyoviona muumini huyo. Mchungaji na shuhuda wa tukio hilo waliamu akuripoti tukio hilo kwa majirani na serikali ya kijiji hicho.


Tukio hilo la namna yake limewaunganisha wachungaji na waumini wa makanisa zaidi ya matano na kufanya Ibada ya pamoja kwa ajili ya maombezi katika eneo hilo.
Kwa upande wao wachungaji waliofanya mahojiano na blogu hii wanazungumziaje tukio hilo? 
Bofya hapa uwasikilize....
wachungaji na waumini kwa pamoja leo walikubaliana kuchoma moto vitu hivyo, lakini serikali ya kijiji hicho imewazuia wasichome moto leo na hivyo kuwataka kesho wachome mto vitu hivyo kwa kushirikiana na serikali ya kijiji hicho.

Nao mashuhuda walioshuhudia maajabu hayo wametoa ushuhuda wao na kuwaasa watanzania kumtegemea Mungu kwa moyo wote na kwa kila jambo kwa kuwa siku za mwisho zimekaribia.

Moja ya mashuhuda hao Lone Mkono amesema matukio kama hayo yanaashiria mwisho wa dunia na kuwataka wakristo wasife moyo kwa sababu ya majaribu wanayo yapata.
Kwa mjibu wa mchungaji mwenyeji wa kanisa hilo amesema mara nyingi kanisa hilo tangu lijengwe limekuwa likiangukaanguka kuta zake mara kwa mara, hivyo na tukio hilo ameliunganisha na matukio mengine yanayolikabili kanisa hilo kuwa ni mipango ya shetani kutaka kulirudisha nyuma kanisa hilo.
Bofya hapa kupata sauti za mashuhuda wachungaji na mchungaji mwenyeji kasema nini