NGUVU YA HABARI

Sunday, December 22, 2013

FILIPO PHIRI: Nguo fupi, matiti nje, milegezo marufuku walokole

A
skofu msaidizi wa Jimbo la Kinondoni na Mchungaji  wa kanisa la EAGT Mikocheni ‘A’ Filipo Phiri apiga marufuku kwa waumini wote uvaaji wa nguo fupi, mlegezo na unyanyuaji matiti kwa wanawake na mavazi yasiyoendana na misingi ya dini pamoja  na utamaduni wa Mwafrika, asema yarudisha nyumba Injili ya Kristo.
Akihutubia waumini wa kanisa hilo lililopo Samaria Mikocheni A Desemba 22 mwaka huu, mchungaji Phiri alisema wakristo wanaovaa nguo fupi hawana nia ya kukuza injili kwa mataifa zaidi ya kuwaingiza majaribuni waumini wenzao na hata mataifa wanaotaka kuwahubiria na hivyo kuwa kikwazo katika kueneza injili ya Yesu Kristo kwa Mataifa.
Aliongeza kuwa wanawake wanatakiwa kuvaa nguo fupi (nusu uchi) wakati wakiwa na wanaume zao  katika maandalizi ya tendo la ndoa na si kuvaa nguo fupi kanisani kila mahali kwa kuwa huhizi heshima zao.
Pia, mchungaji Phiri alikemea tabia ya wanawake kunyanyua matiti yaonekane juu kwa madai kuwa (wasichana) wengi hawataki yaonekane matiti yao yameanguka (yamelala) jambo ambalo mchungaji alidai limekuwa likiwaingiza vijana majaribuni kwa kuwatamani wasichana hao pindi wakiyaangalia matiti (maziwa) ya wanawake hao.
“Tabia ya kuacha maziwa yenu yaonekane kwa watu, na kunyanyua maziwa yenu kwa kuvaa kanchiri (sidiria) ndogo si desturi yetu walokole wala Waafrika bali mmeiga tu.
“Nikimwona mwanamke amevaa nusu uchu au nguo vupi, amenyanyua maziwa kuwatega vijana wangu nitamfukuza mbele ya kanisa hata kama yupo kutoa sadaka madhabahuni,” alisisitiza mchungaji Phiri.
Aidha Mchungaji Phiri aliwataka vijana wanaovaa suruali mlegezo maarufu kata ‘K’ kuacha tabia hiyo mara moja vinginevyo nao atawafukuza kanisa akidai kuwa nao wanazui in jili ya Yesu Kristo isisonge mbele kwa kuwa mlegezo huvaliwa na watu wasiokoka na waliokosa heshima mbele za watu.
“Nikikuona umevaa mlegezo makalio yako yanaoneka ama chupi yako inaonekana, I cannot tolerate you, I chase you out (siwezi kukuvumilia, nitakifukuza),” mchungaji Phiri aliwasisitizia vijana waliookoka.
Hata hivyo, mchungaji Phiri aliwataka wanaume kukaa na wake zao na kuwaonya juu ya mavazi wanayovaa mbele za watu na kuwaambia kuwa wajue kuwa mwanamke anatakiwa kuonesha mapaja, maziwa yake kwa mwanamume wake tu, na kwa watu wengine mwanamke anatakiwa kusetiri mwili wake kwa mavazi.
Vivyo hivyo, kwa wanaume aliwatakiwa kutoacha vifua wazi, kuvaa kaptura akidai kuwa si tabia ya watu waliookoka kuvaa mavazi yayowavunjia heshima mbele za watu.
Hayo yote aliongea wakati akifundisha somo la MSIMAMO WA WOKOVU akisoma Mathayo 7: 24-27, Yuda 1:3-5 na 1Wakorintho 2:4-8
Bofya link hii ukitaka sauti
https://soundcloud.com/user442431332/filipo-phiri-nguo-fupi-matiti

No comments: