NGUVU YA HABARI

Thursday, December 27, 2012

Uchumba ni Mkataba na Ndoa ni Agano.

Ndoa ni agano ambalo mtu akisha kuaga ama kusaini makubaliano ya kuoana hayo, haruhusi kumwacha mke ama mume, lakini uchumba  ni makubaliano ya awali ambayo msichana na mvulana hukubaliana kwa malengo ya kuja kuoana baadaye.
makubaliano haya huwa ni mkataba wa watu wawili na makubaliano hayo husainiwa kama wa mkataba ikiwana na maana kwamba mmoja akimchunguza mwenzake wakati wa uchumba akagundua kuwa ana kasoro na hawezi kumfaa katika ndoa, huamua kuvunja mkataba huo na kutafuta mwingine.
lakini mume ama mke akimwacha mwenzake na kuolewa na mwingine ama kuoa mwingine huitwa mzinzi na huhesabika ametenda dbambi.

lakini zifuatazo ni sababu zinazo changia kuvunjika kwa uchumba:                                           

1. Kukosekana kwa uaminifu na uvumilivu kwa wachumba wenyewe katika mahusiano yao. Pindi wachumba hawa wanaposhindwana kuaminiana na kuvumilia, kati yao mmoja huamua kutafuta akiba ama service account na kumwona mwenzake kama hafai tena bila kumshirikisha katika masuala anayoona hayeendi sahihi katika mahusiano yao. Uongo hutawala na sababu nyingi zisizo za msingi ambazo hufungulia mlango wa shetani kuwashambulia na hatimaye uchumba kuvunjika.

2. Uchumba wa mali ama uchumba wa mwenye nacho tu: Kama wachumba hao wanakuwa wamependana kwa sababu mmoja wao anauwezo fulani wa mali ambao umeshawishi mmoja wapo akubaliane na kuwa na mahusiano ya uchumba, pindi mmoja huyo anapofilisiki basi hatima ya uchumba huo huvunjika na mwenye roho ya kutamani watu wenye  nacho basi huanza kupepesa macho na kumtafuta mtu mwingine mwenye nacho. 

Hali ya kutamani maisha makubwa ambayo ni nje na uwezo husababisha uchumba kuvunjika na wakati mwingine akijitokeza mtu mwingine ambaye anaonyesha dalili fulani za kuwa na mali au pesa zaidi ya yule mchumba huchangia kuvunjika kwa uchumba  hivyo ni vizuri kulidhika na mchumba wako na mwenzi uliyenaye kwani MUNGU atawabarikia mkiwa pamoja.                                             

 3.Kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa (katika kipindi cha uchumba). Mara nyingi wachumba wengi wanapendas kufanya ngono katika kipindi cha uchumba hali ambayo huhatarisha mahusiano ya wachumba. kwa maana mtu anayefanya ngono kabla ya kuolewa ni sawa na mtu anayeonjesha parachichi mojawapo kati ya maparachichi anayouza ili mteja aonje utamu wa maparachichi hayo, na akisha kuonja parachichi hilo huwa hanunui lile alilo onja badala yake hununua ambalo hakijaonjwa. Vivyo hivyo mwanamke anayefanya ngono kabla ya ndoa ni rahisi kuachwa ukilinganisha na yule anayetunza kiapo.

Kumbuka uasherati ni dhambi na pia kufanya ngono kabla ya ndoa kunasababisha watu kuzoeana na kumtambua udhaifu mwenzake na hivyo kuamua kuvunja uchumba na kumtafuta mwingine kwa kigezo kuwa atampata mwenye afadhali kuliko wa kwanza.

NI DHAMBI KWA WACHUMBA KUFANYA TENDO LA NDOA KABLA YA NDOA

4.Kujitangaza mapema kwa watu kabla ya wakati muafaka. kujitangaza kwa wachumba kwa jamaa zao kabla ya muafaka, hutoa fursa kwa baadhi ya watu kuzua maneno ya uchonganisha na ya kukatisha tamaa kati ya hao wachumba.

Mfano, wafi watarajiwa wanaweza kumwambia kaka yao amechagua mwanamke asiye na mvuto ama ana sura ya kufukuza watu halia ambayoa kama mwanaume hana msimamao wa kuwakemea dada zake ama marafiki zake, basi huamua kuachia ngazi, vivyo hivyo kwa mwanamke na huchezeshwa sebeni na wasichana wenzake wenye husuda naye ama kila mtaa wanajua yaani kila mtu anajua hii husababisha mmoja ya wachumba kuona kuwa huyu mwenzangu hana siri na hawezi kutunza mambo huenda hata tutakapooana hataweza kutunza siri.

hivyo huchukua hatua ya kuvunja uchumba na wakati mwingine kusemasema kabla ya muda huwasababisha wale walio maadui zenu kuwazunguka kwa mbele na kupindua mathalani marafiki wa karibu wana weza kuzunguka na kukugeuzia kibao hatimaye mjoja wapo hikuta rafiki anamshawishi avunje uchumba na  ya siku chache huyo huyo mshauri anamvisha pete mchumba wako. 

5.Kufuata ushauri bila kuupima na kutomsikiliza MUNGU. Hii inaweza kusababisha  uchumba kuvunjika. ni vizuri kujifunza kumsikiliza MUNGU juu ya yule aliye kuongoza kwamba atafaa kuwa mwenzi wako wa ndoa badala ya kuwasikiliza watu wanasema nini juu ya wewe na mchumba wako. watu wanaweza kumtoa kasoro mfano mchumba mwenyewe hajasoma,ni mbaya,hana figa nzuri,mchafu,hamuendani, maskini na kasoro nyingi tu na hiyo husababisha uchumba kuvunjika                                                     

6.Kuparamia uchumba bila kumhusisha MUNGU. Watu wameonana siku moja na kutamaniana bila kuchunguzana ama kumhusisha MUNGU wanachumbiana. Baada ya muda mfupi wanatangaza mipango ya kuoana kwa kwa watu. Na pindi mmoja wapo anapogundua kuwa walikurupuka basi wala MUNGU hakuhusika kabisa  katika mchakato mzima wa uchumba wao, basi matokeo yake uchumba huvunjika. 

7.kutumia muda mwingi katika uchumba kabla ya ndoa. Kuna baadhi ya wachumba wanatumia muda mwingi sana kukaa katika mahusiano ya uchumba kwa malengo ya kusomana tabia au kuchunguzana au kusubiriana katika masomo nk. Hali hii hupelekea kuchokana katika mahusiano na kuwasababishia kuona kama huenda labda nilichagua mtu asiye sahihi. Baada ya kusoma na madhaifu mengi kwa muda mrefu mwisho uchumba huweza kuvunjika.                                                                                                      

8. Kutofautiana kwa imani ama Dini: Aidha wachumba wanaochumbia wenye msimamo tofautiwa dini husababisha uchumba wao kuvunjika pindi mmoja wapo anapogoma kuhamia kwenye dini ya mwenzake.

9.Upinzani wa shetani ili ukose kilicho bora zaidi. Kuvunjika kwa uchumba wakati mwingine kunaweza kusababishwa na ibilisi shetani ambaye ni mdau wa kwanza wa upinzani juu ya mafanikio ya wana wa MUNGU. Ndiyo maana tunahitaji  sana kufunga na kuomba ili kuvunja na kuharibu kazi za shetani na mipango aanayotuwazia sisi katika maisha yetu.

SHETANI ALIWADANGANYA ADAMU NA EVA  KWA SABABU HAPENDI MAFANIKIO KWA WANA WA MUNGU    

10.Uchumba kuvunjika kwa sababu ya mapenzi ya MUNGU.Sio kila kitu kinaweza kusababishwa na shetani, wakati mwingine MUNGU mwenyewe huingilia kati na kusababisha uchumba fulani kuvunjika kutokana na sababu za kimungu ambazo wakati mwingine kwetu sisi sio rahisi kuweza kuzijua kwa haraka mpaka wakati kamili wa MUNGU utimie au kusudi lake kujidhihirisha wazi. Ni vizuri kwetu sisi kama watu wa MUNGU kutafuta mapenzi ya MUNGU na kujua kwamba kuna wakati  MUNGU mwanyewe  anaweza kusababisha uchumba  kuvunjika kwa ajili ya usalama wetu.

MUNGU BABA AKUBARIKI SANA

Kwa nini watanzania waitwe masikini wakati kuna malighafi za kutosha?


Tanzania bara ilipata uhuru mwaka 1961 kutoka mikononi mwa Waingereza, chini ya mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa Waziri Mkuu wa Kwanza. Mwalimu Nyerere aliposhika tu madaraka alitangaza vita dhidi ya  maadui watatu Maladhi, Ujinga na Umasikini ambao maadui hawa walionekana kuwanyanyasa Watanzania.
Kwa kutambua umuhimu wa kupambana na maadui hawa, Mwalimu Nyerere akishirikiana na viongozi wenzake kupanga sera mathubuti za kutokomeza maadui hao.

Kutoa elimu bure kwa watanzania hususani vijana, kuboresha miundo mbinu pamoja na kuboresha huduma muhimu za jamii yaani vituo vya afya na hospitali ni mbinu moja wapo aliyotumia kupigana na maadui hao.

Aidha, alitangaza Azimio la Arusha 1967 iliyoanisha maadili ya viongozi na kujali usawa kwa watanzania wote bila kuweka matabaka ya wenye nacho na wasio nacho yaani mfumo wa Ujamaa.

Ingawa miaka ya 1970 hadi 1980 Tanzania ilianza kuyumba katika mapambano dhidi ya umasiki huku adui ujinga akionekana kupunguzwa kasi.

Mwalimu Nyerere mwaka 1985 aliamua kumwachia madaraka Mzee ruksa, Ali Hassan Mwinyi, ambaye naye alipambana vilivyo na maadui hao, na kumwachia Rais mstaafu Benjamin Wilium Mkapa.
Rais Mstaafu wa Tanzania,Ali Hassan Mwinyi
Mkapa alikuja na sera ya uwekezaji binafsi (Ubinafsishaji) katika harakati za kupambana na maadui hao, ingawa hakutoa matokeo ya mapambanao hayo na kumwachia Rais Jakaya Kikwete ambayo naye anasubiriwa kutoa matokeo ya mapambano hayo.

Kumbuka silaha kubwa ambayo watanzania wanajivunia kuwashinda maadui hao ni kutokana na kumiliki rasilimali nyingi ambazo ni jibu tosha la kuwashinda maadui hao.

Adui umasikini anatokomezwa kwa kutumia vizuri rasimali zilizopo ambazo baadhi ya rasilimali hizo hazipatika nchi nyingine yo yote.

Adui Ujinga anatokomezwa kwa kuboresha tasnia ya elimu ambayo ndiyo ukombozi na silaha kuu ya kumuua adui huyo.

Adui huyu ujinga hawezi kutokomezwa kama tasnia ya elimu haina fedha za kutosha ili kuboresha miundo mbinu pamoja na mishahara ya walimu na wadau wengine wa elimu.

Wakati huo huo, kitega uchumi cha fedha zitakazosaidia kuwaua maadui ni rasilimali zilizopo nchi Tanzania na sio misaada ya nje, kwa maana ‘fimbo ya mbali haiui nyoka’ na ‘Mtegemea cha nduguye hufa angali masikini’.

Tanzania kama nchi nyingi tangu itangaze vita dhidi ya maadui hawa ni takribani miaka 51 imepita, huku jamii ikisubiri kutawazwa ubingwa dhidi ya maadui hao.

Cha kushangaza wakati Tanzania Bara ikisherekea miaka 51 ya uhuru, serikali ilikiri kushindwa kutokomeza maadui hao hususani Umasiki huku ikiwa imekalia silaha za kutosha kumshinda adui huyo, ama kweli ‘kwenye miti mingi hakuna wajenzi’ na ‘upele humwota asiye na kucha’.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, katika mdahalo wa uhuru ulioandaliwa na Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) kwa kushirikiana na ITV na Capital Radio, alikaririwa  alisema ni kweli Tanzania ni masikini na wasomi hawana budi kushirikiana na serikali kutafuta njia za kutokomeza umasikini nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe
Serikali imetangaza vita nyingi dhidi ya adui umasikini ikisahau kuwa vita ilikwisha tangazwa na Mwalimu Nyerere tangu miaka ya 1967 na kinachosubiriwa ni kutangaza matokeo ya ushindi ama kushindwa.

Je, ni kweli Tanzania ni nchi masikini kama inavyo daiwa na serikali? Ukizingati Tanzania ina mbuga za wanyama, Mlima Kilimanjaro na vivutio vya kihistoria kama Bagamoyo, Kalenga na Lugalo (Iringa) ambako haya ni baadhi ya vivutio vya watalii vinavyo iingizia nchi fedha za kigeni.

Umasikini unatoka wapi Tanzania kama Tanzania ina maziwa, bahari, ardhi nzuri kwa kilimo cha mazao na ufugaji?

Je, miaka 51 ya uhuru wa Tanzania bara, elimu inayotolewa vyuoni haiwaandaa wanafunzi kujitegemea na kuisaidia nchi kuikomboa mikononi mwa maadui hao?

Kwa upande wa wasomi wanachuliaje kauli hii ya serikali kusema Tanzania ni nchi masikini?

Prof. Issa Shivji anapingana na kauli ya serikali kwa kuainisha vitega uchumi ambavyo Tanzania inamiliki kama vile madini, na mbuga za wanyama.

Prof. Shivji amedai kuwa Tanzania si masikini ila tatizo linalofanya watanzania waonekana masikini ni serikali kuunda sera thabiti inayosimamia masilahi ya wananchi wa Tanzania na hatimaye imejikuta ikitetea masilahi ya wawekezaji wa kigeni.

Prof. Shivji amesema wachimbaji wa madini wazawa hawawezeshwi na serikali na hatimaye wanapochimba madini huitwa wamefamia madini ya wawekezaji na kuitwa wavamizi.

Mhadhiri wa Kiswahili katika chuo Cha Dar es Salaam, Dr. Martha Qorro anadaiwa kuwa Tanzania ina rasilimali za kutosha ambazo zikitumiwa vema zitawakomboa Watanzania,

Dk. Qorro anadai kuwa watanzania wanashindwa kutumia rasilimali ziulizopo kutokana na serikali kutokuwa na sera inayoeleweka kuwa Lusha ipi itimike kufundishia elimu ya msingi ha vyuo vikuu ili kuwaandaa vizuri wananchi kutumia rasilimali zao kwa manufaa ya Watanzania.

Amesema lugha ya Kiingereza inayotumika kufundishia elimu ya sekondari na vyuo vya kati na vyuo vikuu haimsaidii mwanafunzi kumuuandaa kuja kutumia rasilimali zilizopo kwa sababu ni lugha ya Kigeni na Watanzania walio wengi hawaijui lugha hiyo.

Dr.Qorro napendekeza Lugha ya Kiswahili itumike kufundishia tasnia ya elimu katika nyanja zote ilikumuandaa mwanafunzi aje atoe mchango mkuu wa kutumia rasilimali zilizopo.

Aidha, mwanasiasa wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Esther Wasira, anakanusha Tanzania si nchi masikini kama inavyodaiwa na serikari, kwa kuwa ina rasilimali nyingi ambazo zinaweza kumkomboa mtanzania.

Wasira anaona kinachochangia watanzania waonekane ni masikini ni serikali kushindwa kutokomeza rushwa inayofanywa na baadhi ya viongozi wa serikali na wafanyabiashara.

Amesema serikali imekuwa mtazamiji wa vitendo vya rushwa na kushindwa kuchukua hatua mahususi dhidi ya wahujumu uchumi hao.

Akitolea mfano wa chaguzi za chama tawala (CCM), ambazo mwenyekiti wa taifa wa chama tawala, Jakaya Mrisho Kikwete alikiri akikithiri kutendeka kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa wanawake na hakuna hatua yo yote ambayo imefanyika licha ya Mwenyekiti kutambua vitendo hivyo.

Anaongeza kuwa serikali kushindwa kuwachulia hatua watuhumiwa wa EPA na RICHMOND ni dhahiri ina bariki umasikini uendelee kuwameza watanzania, na kuwanufaisha wahujumu uchumi wan chi.

Aidha, Wasira anaona kukosekana kwa maadili na miiko kwa viongozi ndiko kunako changia umasikini nchini kwa sababu viongozi hawa  wanatanguliza masilahi ya watu wachache.

Watanzania wana nafasi kubwa ya kutokomeza umasikini iwapo watatunga sheria ya wazi ya kuwabana viongozi kwa kuwahoji pindi wanaposhindwa kutekeleza ahadi na kuvuja mali za umma, na kuwachagua viongozi waadilifu ambao wapo tayari kuutumikia umma kwa kutetea masilahi ya watanzania na sio wawekezaji wa kigeni na watu wachache.