NGUVU YA HABARI

Friday, February 28, 2014

KUKOSEKANA KWA ELIMU YA MAZINGIRA KUNACHANGIA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

Na Samwel Mbugi, Iringa
Kukoseka elimu ya mazingira miongoni mwa jamii ni moja ya sababu inayosabibisha kuongeza kwa uharibifu wa mazingira nchini Tanzania.
Licha ya taasisi zinazojishughulisha na utunzaji wa mazingira kuhimiza utunzaji wa mazingira ikiwemo pamoja na kuanzisha kampeni ya kuzuia ukataji wa mistu pamoja na kulima katika vyanzo vya maji mkoani, wananchi wengi mkoani Iringa hawana elimu ya utunzaji wa mazingira hali iliyosababisha kampeni ya kupambana na uribifu wa mazingira mkoani Iringa kutofanikiwa kwa kiwango cha kuridhisha.
Deodata Kayombo ni mmoja wa viongozi wa wa Asasi rafiki kwa Mazingira Tanzania akizungumza na wananchi mkoani Iringa alisisitiza elimu ya mazingira kuendelea kutolewa kwa jiamii ili kuniusuru mazingira na kudhibiti athari zitokanazo na uharibifu wa mazingira.
Uharibifu wa mazingira mkoano Iringa umechangia kuongezeka kwa ukame na kupungua kwa vyanzo vya maji mkoani humo hali iyosababisha kuongezeka kwa uhaba wa maji.
Kayombo alisema tarafa ya Isimani amekumbwa na janga la ukame zaidi ya miaka thelathini kwa sababu ya wananchi wa tarafa hiyo kukosa elimu ya mazingira.
Katika kuhakikiza azma ya kutunza mazingira mkoani Iringa inaendelezwa, shirika hilo la Asasi Rafiki kwa mazingira Tanzania limezindua mpango wa utunzaji mazingira ilikusaidiqa kurudisha hadhi yake mazingira yaliyoathirika na ukame
Naye mkuu wa wilaya ya Iringa mjini, Dr. Dr. Reticia warioba amewaasa wananchi waliofikiwa na mpango huu kuhakikisha wanaonesha ushirikiano mzuri na asasi hiyo kutunza mazingira kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Hata hivyo, biashara ya mkaa imeonekana kushamiri mkoani Iringa hali iliyosababisha ukame na uharibifu mkubwa wa mazingira.  
Moja ya tanuru za mkaa ambayo imekuwa ni miongoni mwa biashara zinazompatia kipato mwananchi mkoani Iringa.

Biashara ya mkaa mkoani Iringa imekuwa ni biashara kuu ambayo upatikanaji wa soko lake ni rahisi ukilinganisha na biashara ya mazao ya kilimo kama vile kahawa, alizeti na mpunga.

Biashara ya mkaa mkoani iringa inajulikana kwa jina maarufu mali nyeusi ikiwa tayari inasafirishwa kupelekwa sokoni. Kutokana kuwepo kwa soko la mkaa wananchi wengi vijiji husasan vijiana hujishughulisha na biashara hiyo

Ukataji wa misitu holela huchangia uharibifu wa mazingira, ili kukamiliana na uharibifu wa mazingira serikali na asasi nyingine hazina budi kutoa elimu kwa jamii.
(Picha zote ni kwa msaada wa tovuti)

Thursday, February 27, 2014

TANZANIA PRISON YAWACHIMBA MKWARA MGAMBO JKT NA SIMBA SC

Na samwel Mbughi, Mbeya
Katibu mkuu wa timu ya Tanzania Prison amezichimba mkwara timu ya Mgambo JKT na timu ya Simba kuwa timu hizo zitegemee kichapo kutoka kwao.
 Akizungumza na mtandao huu katibu wa timu ya Tanzania Prison SADICK JUMBE alisema kuwa wamejianda vyema kukipiga na timu ya mgambo jkt, mchezo utakaotimua vumbi tarehe 02, machi mwaka huu.    
Jumbe aliwaondoa hofu  mashabiki wa timu hiyo na kuwataka kuishangilia timu hiyo kwa morali kubwa kwa kuwa wachezaji wameandaliwa kisaikolojia vizuri na wapo tayari kuipitisha kichapo kwa timu yo yote watakayo kutana nao.
Sanjari na hilo, hakusita kuzungumzia mchezo utakaotimua vumbi tarehe 8 Machi mwaka huu ukizikutanisha Tanzania Prison dhidi ya timu ya simba katika uwanja wa sokoine jijini Mbeya.
 Alisema kuwa simba waende huku wakijua kuwa Tanzania Prison  si timu ile ya zamania ni Tanzania Prison ni timu ya sasa ambayo wachezaji wake wote wanacheza mfumo wa timu na wana morali kubwa ya kushinda katika mechi zake ziliozosalia.
Aidha, Jumbe alisema kuwa mapungufu yaliyokuwa yanaisabishia Tanzania Prison kufanya vibaya kipindi cha nyuma yametafutiwa tiba yake na kocha wa timu hiyo.  
 Hata hivyo, Jumbe amewaasa waamuzi {marefa} watakaochezesha mechi hizo kuzingatia sheria zote na kanuni zote za mpira wa miguu ili kuepuka lawama.
Tanzania Prison msimu huu imeonekana kuanza vizuri baada ya kutotambia na Wagosi wa Kaya Coastal Union na kisha kuwatandika bakora mojo Mtibwa Sugar uwanja wa Manungu hatimaye kuwarusha kwata maafante wanzao bila huruma JK Ruvu magoli 6 kwa yai, na baadaye kutoshana nguvu na timu iliyopo kilele Azam FC yenye point 40 kwa magoli 2 kwa 2.

Timu ya Tanzania Prison ambayo hivi sasa imeanza kuonesha matumaini ya kusalia ligu kuu Tanzania Bara baada ya kuanza vizuri mzunguko wa pili. (Picha kwa msaada wa tovuti)

Msimamo wa ligi kuu Tanzania bara

1(+1)AZAM FC182340
2(-1)YANGA SC172938
3MBEYA CITY19835
4SIMBA SC191632
5KAGERA SUGAR19126
6COASTAL UNION19525
7RUVU SHOOTING18-425
8MTIBWA SUGAR19025
9JKT RUVU19-1322
10PRISONS FC17-317
11MGAMBO SHOOTING19-1717
12(+1)JKT OLJORO19-1514
13(-1)ASHANTI UTD19-1914
14RHINO RANGERS19-1113
Msimamo wa ligi kuu Tanzania bara