NGUVU YA HABARI

Tuesday, December 8, 2015

Wapateni Haki zao Watoto




Wazazi na walezi wametakiwa kuwapatia watoto wao haki za msingi ikiwemo elimu.
Selina Lyapinda ambaye ni mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali Mbeya Women Organisation Prevention of HIV and AIDs alitoa rai hiyo wakati akizungumza na blogu hii Desemba 08 mwaka huu.
Alisema baadhi ya wazazi na walezi huwakatisha masomo watoto wao kwa kuwatumia kama vibarua nafuu wa kuinua uchumia wao, vitendo ambavyo huwanyima watoto haki zao za msingi ikiwemo haki ya elimu.
Mmoja wa wazazi ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema watoto walio wengi hutafuta vibarua wenyewe ili wapate fedha za kujikimu pamoja na kulipa michango shuleni ambayo wazazi wao wameshindwa kuimudu kutokana na ugumu wa maisha.
Wakizungumza na blogu hii baadhi ya watoto ambao wamejiingiza katika vibarua vya kukata majani ya mifugo wamesema walikatisha masomo yao baada ya wazazi wao kukosa fedha za kuwasomeshea.

No comments: